May 19, 2024

Mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo kadhaa ya Kenya na mafuriko makubwa yamesababisha vifo vya watu 169, afisa wa serikali alisema.

Msemaji wa serikali Isaac Mwaura alithibitisha idadi ya waliofariki Jumatatu jioni, akisema bwawa lililopasuka Jumatatu asubuhi katika mji wa Mai Mahiu magharibi mwa Kenya limeua watu 48 na kuathiri wengine wengi.

“Tumepoteza watu 169 tangu mvua kuanza kunyesha. Serikali pia imeimarisha shughuli za utafutaji na uokoaji ili kupata watu ambao wameripotiwa kupotea,” Mwaura alisema kwenye televisheni ya taifa.

Taifa la Afrika Mashariki kwa sasa linakabiliwa na mvua ya juu ya wastani inayotokana na El Nino. Idara ya Utabiri wa Hali ya Hewa nchini Kenya imesema kuwa mvua kubwa itaendelea kunyesha wiki hii, huku kukiwa na uwezekano wa mafuriko na maporomoko ya ardhi katika baadhi ya maeneo.

Mvua kubwa iliyonyesha hivi majuzi imesababisha mafuriko makubwa katika kaunti za Nairobi, Makueni, Pokot Magharibi na Machakos, na kupoteza maisha na mali. Mvua hiyo kubwa pia imekatiza barabara kuu, kutatiza biashara kote nchini, na kulazimu kuahirishwa kwa kufunguliwa kwa shule kwa wiki moja kutoka Jumatatu.

Huku Kenya ikiendelea kukabiliwa na mvua kubwa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres Jumatatu alisisitiza Umoja wa Mataifa itaendelea na ahadi yake ya kusaidia Kenya kufuatia mafuriko mabaya yaliyosababishwa na wiki za mvua kubwa zinazoendelea kuathiri eneo hilo.inkuru yose

Iciyumviro on Mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo kadhaa ya KENYA AFRICA

    David
    May 1, 2024

    Nihatari kweri

    0
    0

Siga Iciyumviro